![]() |
bendera yetu tanzania |
Mfumo wa vyama vingi ni hali ya kuwa na chama zaidi ya kimoja,katika nchi moja.Madhumuni ya kuwa na vyama vingi vya siasa ni kuleta ushindani wa kisiasa,ili kuleta maendeleo ya nchi,upinzani wa kisiasa sio uadui kama watu wengi kwenye nchi zinazoendelea wanavyodhani,kuwa na vyama vingi ni kuongeza wigo wa demokrasia katika jamii huska.
Tanzania ni nchi yenye mfumo wa vyama vingi vya siasa uliorejeshwa katika katiba ya Tanzania mwaka 1992.
Chama tawala ni
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgnse0xRKFUVDRSXrf-h-4BVKYgJGVQkHT8xapOFHlJfNgqLqoLOKecn4oZxBVDgcMWDdBMHWfFv3e12vehjshuTs7NhN1aSLF8Cop2lSCTnI59tzjyE3SsoKf995dgFVivG011oVNWPIwy/s1600/kj.jpg)
Kwa miaka mingi CCM ilikuwa ikifuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Itikadi hii ilipewa nguvu za kisera mwaka 1967 lilipotangazwa Azimio la Arusha. Kutokana na azimio hilo uchumi uliwekwa mikononi mwa umma. Itikadi hii pia ilisisitiza umuhimu wa kuishi pamoja hasa katika vijiji vya Ujamaa.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg_M9_4mgzWP17e5XIlEFz7m3GJpbTPAUYODKWKVvFNM8LdVTJC1EeDk4JZPP8eXGmAr-OPmKhIzgalYDuOhLk9OwiHOD6tzFov2SJjBa3eM3JqYcvpsQhJlM4Hx4yWENmZAYFFYwSWSApr/s1600/mk.jpg)
TANU ilianzishwa Julai 7, 1954 kutokana na Tanganyika African Association (TAA). TAA ilikuwa na mwelekeo wa kitamaduni zaidi ya siasa. Mwenyekiti wa kwanza wa TANU alikuwa Julius Kambarage Nyerere.
TANU ilishinda kila uchaguzi chini ya utawala wa kikoloni ikawa chama cha kuongoza Tanzania hadi ilipopata uhuru wake mwaka 1961. Katiba ya Taifa ya mwaka 1962 ilifanya TANU kuwa chama cha pekee nchini ikifuata mfano wa nchi za kijamaa zenye muundo wa siasa ya chama kimoja.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhtxohw2Fl9SrZXANUPmawOcY6L_utLfnTiwYwUMWy1AMmmop_Tk7dQ5Qr1eTg_TJen5205h_qjkrlJaftu1Fn-qLeMVcZezfSbmZfcD-ZXy5GVkqGuz_lbRzup-7_0GzVGuHc9qqMhkXYM/s1600/nye.jpg)
No comments:
Post a Comment