Sunday, April 1, 2012

UCHAGUZI ARUMERU MASHARIKI

NASARI JOSHUA
     Ni kitimtim arumeru mashariki, ni kivumbi cha uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo hili kwa sababu kuna mvutano mkubwa kati ya CCM chama cha mapinduzi na CHDEMA chama cha demokrasia na maendeleo. kwa matokeo inaonyesha kuwa chama cha mapinduzi kipo chini kulingana na matokeo ya vituo mbalimbali katika jimbo hili la arumeru mashariki hivyo bas chama cha demokrasia na maendeleo kimeonekana kikiongoza katika maeneo mengi ya hapa arumeru mashariki kikiwemo kituo kilichopo katikati ambacho ni usa river. kwa hali hii sina budi kusema kwamba chama cha demokrasia na maendeleo kimeshika kasi na huenda kikawa kidedea na kushika hatamu hii ya uchaguzi mdogo wa arumeru mashariki.


SIOI SUMARI
     nai jambo la kumshukuru mungu kwani uchaguzi umeenda bila vurugu kubwa kama zile zilizo pita katika uchaguzi uliopita. vurugu zimetokea lakin ni kwa kiasi kidogo sana. MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI ARUMERU MASHARIKI.

No comments:

Post a Comment