Monday, May 21, 2012

HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI

  TANZANIA MAJONZI KILA KUKICHA
KATIKA BURUDANI

 Ni masikitiko makubwa sana kwa tanzania kuondokewa na watu maarufu na majembe ambao walikua wakitegemewa na familia zao na taifa kwa ujumla ili waweze kuinua uchumi wa tanzani. kwa sasa nchi ambayo ndio inaanza kupata maendeleo kupotelewa na watu ambao walikua ni chachu ya maendeleo ni pigo kubwa sana.

  hajapita miezi mingi Tanzania tuliondokewa na mtu muhimu msanii mkongwe wa muziki aliekua akivutia sana watalii na watu ndani ya nchi aliekua akianza kujijenga na kupanda chati kwa kasi sana kwa staili yake aliokua akiitumia ulale pema mr Ebo. ni msanii aliekua mcheshi na muelewa kwa kila jambo alilokua akiambiwa....

  haijapita miezi kadhaa tena tukaondokewa na nguli wa filamu tanzania charles kanumba. tutakukumbuka sana kanumba kwa filamu zako zilizokua zinauza sana ndani na nje ya nchi.....









KATIKA MICHEZO
Pia hatujakaa muda mrefu patrick mutesa mafisango katutoka kiungo wa simba sports club ale tegemewa na timu pia mashabiki wa simba katika kuinua simba mpaka kileleni tutakukumbuka patrick na tanahitaji na tutahitaji watu kama wewe ni pengo kubwa uliacha tanzania na tanzania simba sports club.....









                                                                                                                                                               TANZANIA nchi yenye amani na utulivu lakini ni nchi ambayo majonzi hayakauki machoni hatujawasahau kina john mjema,steve 2k,na viongo wa serikali kama kina nyerere,omari ali juma, na wegine wengi tutawakumbuka..... tuombe tanzania iwe tanzania yenye amani na furaha sio majonzi kila kukicha

Monday, April 16, 2012

KILIMANJARO MUSIC AWARDS YATIKISA ILA KWA MAJONZI

  Ni tamasha kubwa ambalo hufanywa kila mwaka kwa kuwapa tunzo wasanii wanaofanya vizuri katika kazi zao na tunzo maalum kwa wasanii ambao walionekana kutoa mchango mkubwa katika muziki wa tanzania. tamasha lilikua ni kubwa la aina yake lilionekana kujaa kwa watu wasanii nao walionekana kuitikia wito wakongwe kwa wachanga.
    


   Lakini tamasha hili liligubikwa na majonzi pindi pale baadhi ya wasanii walipo onyesha kumkumbuka msanii mahiri kwa kutunga na kuigiza filamu na sio katika filamu tu hata katika muziki STEVEN CHARLES KANUMBA. mungu amrehemu. majonzi haya au msiba huu ulionekana kumgusa sana msanii BARNABA pia ilikua ni furaha kwake kwani pindi msanii wa filamu

baba steve
 kanumba alipo fariki ndipo siku hiyo alipo pata mtoto aliempa jina la steve kutokana na msiba huo mkubwa. lakini majonzi hayo ya msanii barnaba yalizimwa baada ya kupata tunzo ya mwimbaji bora wa mwaka.hongera barnaba kwa tunzo na mtoto...

Tuesday, April 10, 2012

NINI KILICHOMUUA STEVEN CHARLES KANUMBA?

jeneza lililo beba mwili wa marehemu kanumba

 
Msanii nyota wa filamu nchini, Steven Kanumba amefariki kutokana na tatizo la mtikisiko wa ubongo linalojulikana kitaalamu kama BRAIN CONCUSSION, taarifa za kitabibu zimeeleza.

Taarifa hizo za ndani, zimepatikana jana baada ya jopo la madaktari bingwa watano wa hospitali ya taifa Muhimbili kuufanyia uchunguzi mwili wa marehem, zimeeleza kuwa tatizo hilo linaweza kumfanya mtu apoteze maisha mara moja au baada ya siku kadhaa.Mmoja wa madaktari hao ambae aliomba jina lake lisitajwe gazetini alisema waligundua tatizo hilo baada ya kumfanyia uchunguzi huo kwa zaidi ya masaa mawili.

"tulianza kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 6:45 mchana na tukagundua kuwa marehemu alifariki kutokana na mtikisiko wa ubongo kwa kitaalamu Brain Concussion" alisema. Kanumba alipata mtikisko huo ambao husababisha kufeli kwa mfumo wa upumuaji (cardio-respiratory failure) "kilichomuua hasa ni mtikisiko wa ubongo, ambao endapo unatokea katika sehem ya nyuma ua ubongo (cerebram), huua kwa haraka" alisema daktari huyo na kuongeza kuwa mtikisiko wa ubongo wa nyuma husababusha matatizo ya mfumo wa upumuaji na hilo limeonekana katika mwili wake.

"Baada ya ubongo wake kutikiswa kwa nguvu, mfumo wa upumuaji unafeli na ndio maana tumekuta kucha za kanumba zikiwa na rangi ya blue, huku mapafu yake yakiwa yamevilia damu na kubadilika kuwa kama maini, hizo ni dalili za kufeli kwa mfumo wa upumuaji"

"Mtu aliepata mtikisko wa ubongo huweza kutokwa na mapovu mdomoni na hukoroma kabla ya kukata roho na ndivyo ilivyokuwa kwa Kanumba kabla hajafariki.

Daktari mwingine alieshiriki katika uchunguzi huo ambae pia aliomba jina lake lisitahwe alisema ubongo wa mwigizaji huyo umevimba na kushuka karibu na uti wa mgongo na hivyo kuathiri mfumo wa upumuaji. Alisema sehemu ya maini na maji maji ya machoni ya marehemu, vimepelekwa kwa mkemia mkuu wa Serikali ili kubaini endapo kuna sumu au kitu kingine katika mwili huo

Saturday, April 7, 2012

JE WAJUA MAJINA YA WAJUMBE WA TUME YA KATIBA YA NCHI (TANZANIA)?



 Ni mh dr: rais jakaya mrisho kikwete akitangaza mabadiliko ya tume ya uundwaji wa katiba mpya ikulu jijini dar es salaam.

ni lazima tujue hatima ya katiba mpya sisi watanzania


TUME YA MABADILIKO YA KATIBA
(Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura 83,Toleo la 2012, Vifungu 5, 6 na 7)
______________________________



ni hatua ya mwanzo katika mchakato wa kuunda katiba mpya
UONGOZI WA JUU

1. Mhe. Jaji Joseph Sinde WARIOBA - Mwenyekiti
2. Mhe. Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino RAMADHANI -  Makamu Mwenyekiti

WAJUMBE KUTOKA TANZANIA - BARA

1. Prof. Mwesiga L. BAREGU

2. Nd. Riziki Shahari  MNGWALI

3. Dr. Edmund Adrian Sengodo MVUNGI

4. Nd. Richard Shadrack LYIMO

5. Nd. John J. NKOLO

6. Alhaj Said EL- MAAMRY

7. Nd. Jesca Sydney MKUCHU

8. Prof. Palamagamba J. KABUDI

9. Nd. Humphrey POLEPOLE

10. Nd. Yahya MSULWA

11. Nd. Esther P. MKWIZU

12. Nd. Maria Malingumu KASHONDA

13. Mhe. Al-Shaymaa J. KWEGYIR (Mb)

14. Nd. Mwantumu Jasmine MALALE

15. Nd. Joseph  BUTIKU 
WAJUMBE KUTOKA TANZANIA - ZANZIBAR

1. Dkt. Salim Ahmed SALIM

2. Nd. Fatma Said ALI

3. Nd. Omar Sheha MUSSA

4. Mhe. Raya Suleiman HAMAD

5. Nd. Awadh Ali SAID

6. Nd. Ussi Khamis HAJI

7. Nd. Salma MAOULIDI

8. Nd. Nassor Khamis MOHAMMED

9. Nd. Simai Mohamed SAID

10. Nd. Muhammed Yussuf MSHAMBA

11. Nd. Kibibi Mwinyi HASSAN

12. Nd. Suleiman Omar ALI

13. Nd. Salama Kombo AHMED

14. Nd. Abubakar Mohammed ALI

15. Nd. Ally Abdullah Ally SALEH


UONGOZI WA SEKRETARIETI

1. Nd. Assaa Ahmad RASHID -  Katibu
2. Nd. Casmir Sumba  KYUKI -  Naibu Katibu 

TUTAMKUMBUKA MILELE STEVEN KANUMBA

MAREHEMU STEVEN KANUMBA




 Ni miaka ishirini na nane hivi sasa tangu kuzaliwa kwa nguli wa filamu tanzania (STEVEN CHALSE KANUMBA) imepita tangu mnamo mwaka 1984-2012. tarehe saba mnamo majira ya saa nane usiku ndipo yalimkuta mauti muigizaji steven kanumba.




ENZI ZA UHAI WAKE (STEVEN KANUMBA)



    Ni jambo la kusikitisha sana kwani ni kifo cha ghafla sana kutokea kwa msanii nyota kama huyu, pia ni jambo la kushtusha sana kwani ni kijana mdogo ambae anategemewa na familia yake. si familia tu pia taifa zima linamtegemea kwa kiwango kikubwa sana kwani ni muelimishaji jamii mzuri pia ni mmoja wa vijana ambao huingiza kipato kikubwa katika uchumi wa nchi yetu. 





ELIZABETH MICHAEL (LULU)




     KWA MUJIBU WA MDOGO WA MAREHEMU STEVE KANUMBA, ALISEMA KUWA ELIZABETH MICHAEL  MAARUFU KAMA LULU ALIKUJA NYUMBANI KUKAWA NA KAUGOMVI  AMBAPO WAKAINGIA CHUMBANI WAKIWA HUKO BAADA YA MUDA,LULU ALITOKA NA KUMUITA YEYE  KUMUAMBIA KANUMBA KAANGUKA, YE ALIPOENDA AKAMKUTA KAANGUKA NDIO AKAENDA MUITA DAKTARI WA KANUMBA AMBAPO ALIPORUDI HAKUMKUTA LULU, LAKINI  HADI TUNAVYOONGEA LULU YUKO POLISI OSTERBAY KWA AJILI YA MAHOJIANO NA POLISI, NA MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA MUCHUARI MUHIMBILI. 
   
   BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA , KAMWE HATUTO MSAHAU STEVEN KANUMBA KWA KAZI YAKE NA UCHESHI WAKE MUNGU AMREHEMU NA AMUWEKE MAHALI PEMA PEPONI AMEN.........

Wednesday, April 4, 2012

JOSHUA NASARI PHYLOSOPHY KABLA NA BAADA YA USHINDI WA KISHINDO

Tumeanza na Mungu, tutamaliza na Mungu – Joshua Nasari

“Cha kwanza kabisa namshukuru sana Mungu ambaye alinipa maono ya kuwa mbunge wa Arumeru mashariki, nimekuwa nikiyasema kwa muda mrefu watu walifikiri natania, lakini vilevile nikishukuru chama changu cha CHADEMA ambacho kilinipa ridhaa ya kusimama kuwakilisha kwenye uchaguzi mdogo wa Arumeru mashariki, kwakweli niwashukuru sana watu wa Arumeru mashariki ambao hawakujali umri wangu, hawakujali uwezo wangu kifedha, hawakujali historia ya familia yangu katika siasa, hawakujali kila mapungufu ambayo nilikuwa nayo, lakini wakaamua kunichagua…..napenda niseme  na kama nilivyosema tangu mwanzo kwamba tumeanza na Mungu na tutamaliza na Mungu na siyo kwenye kupata kura peke yake, tutaendelea kumtumikia Mungu na kumuweka Mungu mbele, tutamtanguliza yeye na tutaongozwa na yeye siku zote”

Haya ni maneno ya mbunge wa CHADEMA mtumishi wa Mungu, Joshua Nasari (26) aliyeshinda Jimbo la Arumeru mashariki kwa kura 32972 ambazo ni sawa na asilimia 54 na kufuatiwa na mgombea wa chama cha mapinduzi, Sioi Sumari aliyepata kura 26,757 sawa na asilimia 42.

Sunday, April 1, 2012

UCHAGUZI ARUMERU MASHARIKI

NASARI JOSHUA
     Ni kitimtim arumeru mashariki, ni kivumbi cha uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo hili kwa sababu kuna mvutano mkubwa kati ya CCM chama cha mapinduzi na CHDEMA chama cha demokrasia na maendeleo. kwa matokeo inaonyesha kuwa chama cha mapinduzi kipo chini kulingana na matokeo ya vituo mbalimbali katika jimbo hili la arumeru mashariki hivyo bas chama cha demokrasia na maendeleo kimeonekana kikiongoza katika maeneo mengi ya hapa arumeru mashariki kikiwemo kituo kilichopo katikati ambacho ni usa river. kwa hali hii sina budi kusema kwamba chama cha demokrasia na maendeleo kimeshika kasi na huenda kikawa kidedea na kushika hatamu hii ya uchaguzi mdogo wa arumeru mashariki.


SIOI SUMARI
     nai jambo la kumshukuru mungu kwani uchaguzi umeenda bila vurugu kubwa kama zile zilizo pita katika uchaguzi uliopita. vurugu zimetokea lakin ni kwa kiasi kidogo sana. MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI ARUMERU MASHARIKI.

Saturday, March 31, 2012

DO YOU KNOW TAARAB MUSIC IN TANZANIA?



          Taarab, also called tarabu or tarab, is Zanzibar's most popular music. Taarab is popularly known as Swahili wedding music, since taarab musicians and music are an essential part of these multi-day festivities. The east African coast has served as a center for trade with countries throughout the Middle East and Asia, and taarab music reflects many of the cultures which have passed through this region.
Through its years of development, taarabu has been an exceptionally inclusive art form, adapting and incorporating elements from Swahili, Arabic, Indian, Egyptian, and other cultures. This can be seen in the range of instruments used in taarab ensembles and orchestras which include Middle Eastern oud and dumbek, Indian tabla, western electric keyboards, and the Japanese taishokoto (described as a "banjo/typewriter-key hybrid"). Similarly, taarab rhythms reflect traditional ngoma dances like chakacha, Indian film scores, Cuban rumba, and various Zairean and East African dance music. Perhaps most importantly, taarab lyrics radiate with the allusive intricacies of Swahili poetry and showcase the beauty of this long, literary tradition.
The word taarab is of Arabic derivation and contains multi-layered meaning. Gilbert Rouget in Music and Trance explains taarab comes from "the verb tariba which means "'to be moved, agitated'...also signifies 'to excite, to want to move,' and hence 'to sing, to make music." Historically, taarab was first introduced to Zanzibar in 1870 by the Sultan Seyyid Barghash who brought a group of Egyptian musicians to his court. Barghash sent a Zanzibari musician, Ibrahim Muhammed, to study in Cairo and upon his return he formed the Zanzibar Taarab Orchestra. In 1905, Zanzibar's second music society, Ikwhani Safaa Musical Club, was established and continues to thrive today with around 35 active members. Ikhwani Safaa and Culture Musical Club (founded in 1958) remain the leading Zanzibar taarab orchestras.
Taarab's first modern superstar ascended in 1928 with the Swahili singer Siti bint Saad who appeared on hundreds of 78's, many of them recorded in India. Unlike the majority of taarab which was sung in Arabic, Saad sang in Swahili and presaged a change in the direction of the music. After her death in 1950, taarab lyrics became prominently Swahili, and more female singers appeared with formerly all-male musical clubs. Another dramatic turn occurred with the revolution of 1964's political push to de-arabacize the island and its cultural institutions. Some taarab clubs switched from Arabic to Swahili names, (although many have reverted back), and musical societies were fully opened to women members.




Walipewa cheti cha PF90kwa ajili ya kupeleka kwenye ofisi za BIMA kwa ajili ya ukarabati wa magari yote yalio pata ajali (yaani gari langu na la kwao )

   mimi nilikua nikifanya kazi katika kampuni moja ilioitwa ISI-H engenearing company limited, kwa kifupi ilijulikana kama (I E C L) nilikua kama msaidizi kwa lugha ya kigeni ni secretary wa kampuni ile iliokua ikifanya kazi maeneo ya nduli kama kilometa tano kabla kufika kwenye kiwanja cha ndege cha nduli.

   kampuni ile ilikua ikitengeneza barabara ile iliotoka iringa  mjini hadi mkoa wa dodoma kwa kiwango cha lami. ama kweli niliamini msemo wa wahenga usemao "fimbo ilio mkononi, ndio iuayo nyoka". kuna msaidizi wangu kazini alipoona sirudi kazini kwa muda tuliopewa kwenda kupata mlo wa mchana, alijaribu kudadisi ni nini kimetokea kwangu mpaka muda ule sijarudi kazini na alipo gundua niliondoka na gari na kukutana na mwanamke yule niliemsaidia kwa kuzidiwa kuzimia na kumpeleka hospitali;


Tuesday, March 27, 2012

BONGO BILA SKENDO



                                     Naomba niongele skendo za wasanii bongo kwa uchungu na hisia ambazo naziona katika jicho langu la tatu. si mara moja au mara mbili kumekua kukitokea skendo za wasanii wa bongo kuchafuana wenyewe kwa wenyewe,wasanii kwa wahandishi wa habari bega kwa bega kufuatiliana. hivi ni vyema kwa wasanii kurukaruka kama kima na kufanya mambo ya ajabu na kuweka maswali kwa vichwa vya watu chungu mzima. hii inatokana na nini mimi nadhani ni ukosefu wa maadili kwa wasanii wa sasa.

 hivi ni kitu gani kinacho wafanya muache kufanya mambo ya kazi zenu na kufanya uzinzi hadharani, starehe zilizopindukia.

enyi wasanii acheni hayo mambo mna dhalilisha heshima ya nchi tanzania na pia hamjengi picha nzuri kwa jamii inayo wazunguka na kuwasikiliza kama wasanii.

 wasanii badilikeni ili muwe fundisho zaidi kwa jamii inayo wazunguka  na hii itafanya muheshumike na muonekane watu ambao wana mchango mkubwa katika jamii....BONGO BILA SKENDO INAWEZEKANA..

JE VYAMA VYA SIASA VILIANZIA WAPI?

bendera yetu tanzania



Mfumo wa vyama vingi ni hali ya kuwa na chama zaidi ya kimoja,katika nchi moja.Madhumuni ya kuwa na vyama vingi vya siasa ni kuleta ushindani wa kisiasa,ili kuleta maendeleo ya nchi,upinzani wa kisiasa sio uadui kama watu wengi kwenye nchi zinazoendelea wanavyodhani,kuwa na vyama vingi ni kuongeza wigo wa demokrasia katika jamii huska.
Tanzania ni nchi yenye mfumo wa vyama vingi vya siasa uliorejeshwa katika katiba ya Tanzania mwaka 1992.
Chama tawala ni    

      Chama cha Mapinduzi (CCM) ni chama tawala nchini Tanzania. CCM ilizaliwa 5 Februari, 1977 baada ya kuungana kwa vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) kilichokuwa kikitawala Tanzania Bara na Afro-Shirazi Party (ASP) kilichokuwa chama tawala cha Zanzibar wakati huo. Chama cha Mapinduzi kilikuwa kikiongozwa na Mwalimu Nyerere na Afro-Shiraz Party kilikuwa chini ya Amaan Karume.
Kwa miaka mingi CCM ilikuwa ikifuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Itikadi hii ilipewa nguvu za kisera mwaka 1967 lilipotangazwa Azimio la Arusha. Kutokana na azimio hilo uchumi uliwekwa mikononi mwa umma. Itikadi hii pia ilisisitiza umuhimu wa kuishi pamoja hasa katika vijiji vya Ujamaa.

Tanganyika African National Union (TANU) kilikuwa chama kilichotawala Tanganyika na Tanzania hadi muungano wa chama hiki na Chama cha Afro-Shirazi cha Zanzibar ulipounda Chama cha Mapinduzi (CCM) mwaka 1977.
TANU ilianzishwa Julai 7, 1954 kutokana na Tanganyika African Association (TAA). TAA ilikuwa na mwelekeo wa kitamaduni zaidi ya siasa. Mwenyekiti wa kwanza wa TANU alikuwa Julius Kambarage Nyerere.

TANU ilishinda kila uchaguzi chini ya utawala wa kikoloni ikawa chama cha kuongoza Tanzania hadi ilipopata uhuru wake mwaka 1961. Katiba ya Taifa ya mwaka 1962 ilifanya TANU kuwa chama cha pekee nchini ikifuata mfano wa nchi za kijamaa zenye muundo wa siasa ya chama kimoja.


Afro-Shirazi Party (kifupisho: ASP) ilikuwa chama cha siasa kisiwani kwa Zanzibar. Ilianzishwa wakati vyama viwili vingine, yaani Shiraz Party ya Waajemi na Afro Party ya Waafrika, vilipoungana. Uanzishaji wa chama hilo ukasababisha uondoaji wa Waarabu kutoka utawala wa Zanzibar katika mapinduzi ya mwaka wa 1964. Mwaka wa 1977, ASP ilijiunga na TANU kuwa Chama cha Mapinduzi.

Saturday, March 10, 2012

JE WAIJUA NDOTO YA BARNABA

BARNABA
Toka nyumba ya kukuza vipaji ya THT, Barnaba alikuwa na kifua cha kuweka wazi kuwa moja ya mikakati yake mikubwa ilikuwa ni kugonga kazi moja na bishoo mkongoman  Fally Ipupa.
Lakini maneno ya Barnaba hayakuwa ya bure tu kwani yalitokana na MkongoMan huyo kumfagilia Barnaba kwenye ukurasa wake wa Twiter kuwa anafurahishwa na kazi za bwana mdogo huyo toka Bongo na kuahidi kuwa ipo siku atafanya nae kazi.
Hapa ananukuliwa Fally toka ukurasa wake wa Twitter;
"Nimeridhishwa na kiwango cha mwanamuziki kutoka Tanzania Barnaba na nina nia ya kufanya nae kazi atakapokuwa tayari"ni baadhi ya maneno yalivyosomeka kwenye ukurasa wa Twiter wa mwanamuziki huyo kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo.
KILICHOJIRI WAKATI WA ZIARA YA FALLY IPUPA MWISHONI MWA WIKI ILIYOPITA
Taarifa rasmi ni kwamba kolabo hiyo inafanywa wiki hii na itarekodiwa katika studio za THT Dar es salaam.
Barnaba mwenyewe anaweka wazi kuwa litakuwa ni songi la mahaba litakaloitwa 'TUACHANE KWA WEMA',
Akiendelea kufunguka, Barnaba anasema kolabo hilo amelipata free kabisa bila kumlipa Fally hata shilingi 100, na hii ni kutokana na bishoo huyo wa kikongo kuzimikia kazi za Barnaba tangu muda mrefu.
Hii kolabo inafanyika miezi mitatu baada ya Fally Ipupa kukubali kupitia twitter kwamba anamjua na anakubali uwezo wa BARNABA na yuko tayari kufanya nae kolabo.

HISTORY OF WAYNE ROONEY

Wonder boy Wayne Rooney is the name Wayne Rooney first premiership goal against Arsenalon everybody's lips as Roo-mania sweeps across the country. At the tender age of 16, Rooney announced himself to the Premiership as a top prospect - scoring a seamless goal against Arsenal to earn his first victory for Everton in the last minute of the game.

Wayne Rooney is a born and bred Liverpudlian. The son of a working-class family, he grew up in the suburb of Croxteth. Brought up in a three-bedroom council house with his parents, Jeanette and Wayne, and his younger brothers, Graham and John, young Wayne had not much more than the dreams of every other little boy in his town. His mum Jeanette was a dinner lady at a local school. The family have always been Everton-mad, and Rooney's old bedroom window, which was visible from the street, was filled with Everton pennants.

Rooney was the talk of the town well before his Wayne Rooney Everton shirt presentationinternational success. He was only nine when he was spotted by Everton scout Bob Pendleton playing for boys' club Copplehouse in the local Walton and Kirkdale Junior League. In his last season with them he scored 99 goals before joining the Everton academy. His progress was so swift that he was playing for the Under-19s side when still only 15.

His life now is very different, though his superstardom Wayne Rooney girlfrienddoesn't look like it's gone to his head, he still looks like the boy next door, and if you passed him on the street you wouldn't look twice, he certainly doesn't carry the glamour of Beckham, but who cares? As long as he keeps scoring the goals, he's a national hero.

Wayne Rooney is the top goal scorer in Euro 2004, and has Wayne Rooney first England Goal against Australiabeen describes by England coach Sven-Goran Eriksson as the greatest teenage talent to emerge at a soccer tournament since Pele at the 1958 World Cup. Still at only 18 his career has just started, Liverpool-born Ronney is a boy that everyone wants to be.
Wayne Rooney joined Manchester United on Tuesday, 31 August 2004 despite a last minute holdup caused by his broken foot. Manchester United finalized the deal to acquire the 18-year-old striker from Everton at the transferWayne Rooney Manchester United deadline date. The six-year deal is worth $48.3 million; with agent fees, the total soars to $54 million. "It was a tough decision to leave Everton, the club I've supported and played for all my life, but I'm excited to be joining a club as big as Manchester United," Rooney said in a statement released by his new team. "I feel this can only improve my career, playing with top players in top competitions like the Champions League and I can't wait to meet up with the team."
 
SEHEMU YA PILI
Lori lile lilituvaa na lenyewe likakita katika ukuta wa mlima ule na gari letu liliingia bondeni na kupinduka na kuvunjika vioo vyote. Sikuumia sana, nilichubuka kwenye mikono yangu na usoni kidogo kwa vioo vile vilivyo vunjika.

Masikini mwanamke yule alikua amechubuka kiasi na alikua amezidiwa kabisa kiasi cha kutoa povu mdomoni. Nilimuonea huruma huku nikijilaumu mwenyewe. Kwani nilihisi mimi ndie nilie msababishia yote hayo. Nilidhani amefariki kwani alitoa povu jingi sana mdomoni na puani mwake. Mimi nilikua mwenye fahamu na nilijitahidi kujinasua kwenye gari hili lililo pinduka ili nikitoka nimtoe na mwenzangu lakini ilishindikana kabisa kwani gari lile lilikua lime bonyea sana.

Bila kutegemea nilisikia sauti ya gari lililopiga kelele ya kuashiria kuna hatari imetokea. Lilikua ni gari la hospitali  kuu ya iringa ilio julikana kwa jina la “government hospital” lilikua na daktari mmoja na wauguzi wawili vilevile liliongozana na gari la polisi aina ya land rover lenye namba PT 220 lililokua na polisi sita.

Polisi wale walijitahidi kutung’oa kwenye adha ile na kutuweka kwenye gari maalum la wagonjwa na kutupeleka katika hospitali kuu ya mkoa wa iringa. Polisi wale watatu kati yao walikua ni polisi wa usalama barabarani na wengine watatu walikua wakitoka katika kikosi cha kutuliza ghasia (FFU).

Tulifikishwa katika hospitali ya mkoa wa iringa ilikua ni majira ya saa saba na nusu mchana. Tulitibiwa lakini mimi nilipata ahuweni haraka kwasababu nilikua sina majeraha mengi. Baada ya siku mbili niliruhusiwa kwenda nyumbani, mwenzangu alikua bado yupo kwenye hali mbaya na aliwekewa mipira ya kuongezewa maji kwenye mishipa yake ya mikono. Nilimuuliza daktari kua ni kiasi gani cha fedha kimetumika kututibu na ni nini kinahitajika kwa wakati huu ili niweze kulipa kila kitu. Kwa wewe unahitaji kulipa elfu kumi na mbili za matibabu yote tulio kutibia na mwenzako bado mpira mmoja wa maji na dawa ambazo atakunywa baada ya kumaliza mpira huo wa maji ambapo gharama ya vitu vyote hivyo ni shilingi elfu thelathini na tano pesa taslimu za kitanzania “alisema daktari ambae alifahamika kwa “doctor huruma Jordan”. Bila kuchelewa nilitoa pesa katika mfuko wa suruali yangu iliokua imechanika kidogo miguuni na vioo vilivyopasuka baada ya ajali ile na kumkabidhi pesa doctor huruma  Nilimkabidhi kiasi alicho kisema na kumsisitiza amuangalie mgonjwa wangu vizuri mpaka atakapo pata ahueni na kupona kabisa. Dactari huruma alinihakikishia kwa maneno matamu kua nisiwe na hofu mgonjwa atapona na atarudi katika hali yake ya kawaida huku akinishika bega na kucheka na kutabasamu kwa matumaini na akaondoka kwa madaha huku koti lake lenye rangi nyeupe lililong’ara likipepea kwa upepo mwanana uliopiga katika eneo hilo la hospitali.

Katika lori lile lililotugonga kulikuwepo na dereva aliejulikana kwa jina la magia na utingo wa mizigo alieitwa mabavu. Walikua wamebeba matunda aina ya mananasi ambayo walitokanayo makambako katika mashamba ya mfanyabiashara binafsi wakipeleka mzigo huo huko dodoma wilayani mpwapwa.

Wenyewe hawakuumia sana kwani gari lao lilipasuka taa za mbele tu kwa kukita kwenye ukuta ule wa mlima mrefu uliopo kwenye eneo hilo lilipo tokkea ajali hiyo. Dereva na utingo wa gari kubwa walipelekwa lumande kwa kutozingatia sheria za barabarani. Walijitetea kwa kusema kwamba gari lile lilipoteza uelekeo kwa kukosa breki, hapo tulikua hatuna jinsi ya kujitoa kwani tulikua kwenye kona kali na gari letu lilikua likienda mwendo kasi hapo tulijitoa muhanga na ajali ilipotokea ilikua ni bahati mbaya. “alisema dereva wa lori lile”. Walisamehewa kwa kuwekwa lumande siku tatu na kutolewa na kupewa cheti cha PF90 kwa ajili ya ukarabati wa magari yote yaliopata ajali..   USIKOSE MUENDELEZO WA THIS IS MY PAGE........
NEXT WEEK...

Saturday, February 25, 2012

MTUNZI:ISIHAKA SALUM MYANZA
 E MAIL: isihakamyanza@gmail.com
MOBILE NO: 0766937781 or 0654284877
 
                    SEHEMU YA KWANZA
 
Ilikua ni siku ya jumatano ambapo nilimuona mwanamke mmoja ambae sikuweza kumtambua jina kwa haraka. Alikua akitembea katika barabara moja iliokua ya vumbi iliyoitwa DODOMA ROAD iliyopo huko mkoani Iringa. Mwanamke huyo aliekua anaonekana amechoka sana na mwenye matatizo makubwa lakini pia alionekana mwenye majonzi usoni mwake ukimtazama.

Yalikua ni majira ya saa sita mchana ambapo jua lilikua likichoma sana huku mimea ikinyon’gonyea mithili ya mbwa alie tishiwa kupigwa akaogopa na kukalia mkia wake. Wafanyakazi wa serikali na watu binafsi walikua wakijiandaa kwenda kula chakula cha mchana katika mahoteli, migahawa na wengine kwenda majumbani mwao ili kupata mlo huo wa mchana. Wengine pia bila kujali wakiendelea kufanya kazi nzito bila kujali huo ulikua ni mda wa kupata chakula cha mchana, si kwamba walikua hawana pesa ya kununulia chakula? La hasha! Walijali sana kazi kuliko kula, lakini walipo jihisi njaa ndipo nao walipojipatia chakula kukidhi haja ya matumbo yao.

Mimi nilikua kwenye gari dogo aina ya Suzuki nilikua nikielekea kwa mama ntilie tulie mzoea kwa jina la mama sheteshete, tulifupisha jina lake na kumuita mama shete. Nilikua naenda kwa mama shete ili nami nipate mlo wa mchana ili nikidhi haja ya tumbo langu. Hapo ndipo nilimuona mwanamke ambae alikua amechoka sana na alikua katika majonzi. Nilimuonea huruma, kwavile nilikua kwenye gari, niliegesha gari langu pembeni ya barabara ile ambayo ilikua ni yenye vumbi lenye rangi nyekundu. Nilishuka ndani ya gari na kumtazama mwanamke yule  masikini! Alikua amevaa kanga ambayo imechanika na kutoboka  utadhani imeliwa na panya na miguuni mwake alikua amevaa kandambili ambazo zilikua tofauti (dongea) pia zilikua zime chafuka pamoja na miguu yake kwa dongo na vumbi jekundu mithili ya mtu alietoka kuchimba ama kulima shamba angali bado kiangazi. Nilitamani nilie lakini nilibaki nimekodoa macho mithili ya mjusi aliebanwa na mlango.

Ghafla mwanamke yule akiyumba kama mlevi aliekunywa pombe nyingi. Alianguka puu!! Mwanamke yule kama kiroba cha unga ama kifurushi cha nguo. Nilimkimbilia na nilipofika karibu yake nilikuta amepoteza fahamu. Hapo akili yangu haikuwaza tena kwenda kula kwa mama shete. Nilifikiri ni jinsi gani naweza kumsaidia mwanamke yule. Nilimbeba na kumpeleka kwenye gari langu na kuwasha moja kwa moja hadi hospitali iliokua mbali na eneo hilo. Nilienda mwendo kasi kwani niliogopa asije akafa kwani alikua akitoka jasho mithili ya mtualie mwagiwa maji usoni. Nilikua nikimpeleka katika hospitali ya mkoa wa iringa iliopo mjini iringa kwani tulipotoka kulikua hakuna hospitali wala zahanati karibu.

Tulipita kama kilometa tano ndipo tuliikuta barabara ya lami ambayo ilikua karibu na kiwanja cha ndege cha mkoa wa iringa kilichoitwa nduli.

Nilimwangalia mwanamke yule usoni, alionekana ni mtu aliezidiwa sana na jasho lilizidi kumtoka usoni mwake. Nilijawa na hofu sana nikifikiri endapo atafariki nitafanya nini? Nilijiuliza maswali mengi ambayo sikuweza kupata majibu mapema kwa hofu nilio kuanayo. Yule mwanamke ambae sikumfahamu jina alizidi kutokwa na jasho hadi sehemu nilio muweka ikalowana tepe tepe. Nilichukua kitambaa changu kidogo (leso) huku nikishika usukani kwa mkono mmoja na mkono mwengine nikijaribu kumfuta jasho mwanamke yule, bila mafanikio jasho liliendelea kumtoka kwa kasi.

Nilitaka kukata tamaa kwani nilipo muangalia mgonjwa alikua bado hanipi matumaini kama anaweza kupona lakini nilipiga moyo konde na kujipa matumaini ingawa ni matumaini hafifu. Niliongeza mwendo kwa kuamini nikifanya hivyo nitawahi kufika katika hospitali hiyo ya mkoa.

Huku nikiongeza mwendo katika  gari kwa mkono mmoja nilishika usukani na kujaribu kufungua madirisha ya gari hilo kwa mkono mwingine. Baada ya muda takribani dakika tatu mpaka tano baada ya kufungua dirisha lililopo karibu na mgonjwa, nilimuona mgonjwa akijaribu kufumbua macho kwa mbali ingawa bado hali yake haikua nzuri.

Lakini mimi niliona akipata ahueni kwa vile alikua hawezi hata kufumbua macho. Nadhani ule upepo uliokua ukiingia ndani ya gari kwa sababu ya mwendo kasi ulimfanya mgonjwa yule apate ahueni.

Nilijaribu kumuita kwa kusema Halo! Halo! Huku huku nikimtikisa kwa mkono mmoja, lakini hakuweza kuongea wala kuitika, macho yake yali fumba na kufumbua kama mtu alietaka kusinzia angali hataki usingizi.

Nilizidi kwenda mwendo kasi ndipo tulipofika sehemu moja iitwayo mgongo, sehemu hii ina kona kali sana ambazo hutakiwi kwenda mwendo kasi. Nilipunguza mwendo ingawa ni kidogo. Ghafla lilitokea lori ambalo sikujua mapema kwamba limebeba nini. Lori hilo lilitokea mbele yetu katika kona hizo za mgongo na lilikua limewasha taa zote angali ni mchana na lilikua likipiga honi mara kwa mara likionyesha ishara ya hatari na lilikua likiyumba barabara nzima. Lori hili lilipoteza mwelekeo nami sikuweza kulikwepa kwani barabara ilikua ni ndogo,upande mmoja wa barabara ni mlima na upande mwine ni bonde kubwa.
..........................itaendelea